TPA YATAKIWA KUSIMAMIA UBORA WA KOROSHO BANDARINI

0
137

Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile ameuelekeza uongozi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kwa kushirikiana na uongozi wa mkoa wa Mtwara kukaa pamoja na kujadili namna bora ya kufungasha mizigo ya korosho kabla ya kuisafirisha.

Kihenzile ameyasema hayo mkoani Mtwara alipokuwa akizungumza katika mkutano wa wadau kwa ajili ya maandalizi ya usafirishaji wa zao la korosho kupitia bandari ya Mtwara.

Kihenzile pia ameitaka TPA kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa maelelekzo ya Serikali kuhusu sekta ya uchukuzi na kutoa taarifa za mara kwa mara kwa Wizara ya Uchukuzi.