Mafuta yazidi  kupanda bei

0
129

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta zilizoanza kutumika leo Jumatano Oktoba 04, 2023.

Petroli itauzwa hadi Tsh 3,281 ikiwa ni tofauti ya Tsh 68 mwezi Septemba, Diseli hadi kikomo cha Tsh 3,448 tofauti ya Tsh 189 mwezi uliopita na mafuta ya taa Tsh 2,943 kwa mkoa wa Dar es Salaam.