TPA kujenga Bandari ya Mbamba Bay

0
139

Naibu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Juma Kajivara amesema Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) imetangaza zabuni na inakaribia kupata mkandarasi kwa ajili ya kujenga Bandari ya Mbamba Bay iliyopo Ziwa Nyasa.

Mhandisi Kajivara ameyasema hayo mkoani Mtwara alipokuwa akieleza namna TPA imejipanga kuhudumia mizigo kutoka nchi jirani kwa kutumia bandari ya Mtwara wakati ukiendelea na mkutano wa wadau wa kujadili juu ya maandalizi ya usafirishaji wa zao la korosho kupitia bandari ya Mtwara.

Ameongeza, ni matarajio kuwa mizigo kutoka nchi ya Malawi itapita bandari ya Mtwara kisha kuelekea Mbamba Bay ili kufika Malawi, akisisitiza kuwa hiyo ni njia pekee fupi ya kusafirisha mizigo kutoka Tanzania hadi Malawi.