Tuhuma zamtupa Antony nje ya kikosi cha Brazil

0
258

Mshambuliaji wa Manchester United, Anthony amekanusha tuhuma zinazomkabili za kumshambulia aliyekuwa mpenzi wake, Gabriela Cavallin, baada ya habari mpya kuchapishwa na vyombo vya habari nchini Brazil.

“Ninaweza kuthibitisha pasi na shaka kuwa tuhuma hizi ni za uongo,” amesema Antony ambaye ameachwa nje ya kikosi cha Brazil kufuatia tuhuma hizo.

Amesema kuwa anaamini uchunguzi wa polisi unaoendelea utaweka bayana ukweli utakaothibitisha kuwa hana hatia.

Antony ameachwa nje ya kikosi hicho kinachoshiriki michezo ya kuwania kufuzu kombe la dunia mwaka 2026 dhidi ya Bolivia na Peru, ambapo nafasi yake imechukuliwa na Gabriel Jesus.

Jeshi la Polisi nchini Uingereza limesema kuwa lina taarifa za tuhuma hizo na kwamba kwa sasa uchunguzi unaendelea kubaini ukweli wote.