Mashujaa Wamerejea

0
269

Timu ya Taifa ya soka kwa wanaume (Taifa Stars), imewasili nchini leo alfajiri ikitokea Algeria ilipokwenda kucheza mchezo wa mwisho wa kuwania kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2023.

Katika Kundi F, Tanzania imefuzu pamoja na Algeria ambapo mashindano hayo yatafanyika nchini Ivory Coast kuanzia Januari 13 hadi Februari 11 mwaka 2024.