Tanzania na Indonesia kukuza ushirikiano wa kibiashara

0
256

Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Ashatu Kijaji, amekutana na kufanya mazungumzo kuhusu kuendeleza ushirikiano wa kibiashara kati ya Tanzania na Indonesia na Balozi wa Indonesia nchini, Tri Yogo Jatmiko, katika Ofisi ndogo za Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.

Waziri Kijaji amemhakikishia Balozi huyo kuwa Tanzania iko tayari kuendeleza ushirikiano baina ya nchi hizo na iko tayari kuwezesha miradi ya uwekezaji hususani katika sekta ya kilimo, hasa katika uongezaji wa thamani katika mazao ambayo nchi hiyo imepanga kuyaendeleza, kama vile karafuu, ili kuongeza ajira na kipato kwa Watanzania.