Chongolo akagua bwawa na Nsenkwa

0
118

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo @daniel_godfrey_chongolo akisalimiana na Chifu wa kabila la Wakonongo, Michael Kayamba baada ya kuwasili katika jimbo la Katavi.

Chongolo amefika katika jimbo hilo la Katavi kwa lengo la kutembelea na kukagua mradi mkubwa wa bwawa la Nsenkwa linalojengwa kwa ajili ya kuwa chanzo cha maji kwa matumizi ya Wananchi wa vijiji 16 katika halmashauri ya Mlele mkoa wa Katavi.

Mradi huo utakaowahudumia takribani wakazi elfu 68, utagharimu shilingi Bilioni 2.8.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa bwawa hilo Chongolo amewapongeza wote waliobuni mrati huo kwa kusema kuwa wamebuni jambo litakalokuwa na matokeo makubwa na chanya kwa Wananchi.