Waliofariki kwenye tetemeko ni zaidi ya 2000

0
477

Zaidi ya watu 2,000 wamethibitika kufariki dunia na maelfu kujeruhiwa nchini Morocco kufuatia tetemeko kubwa la ardhi kuyakumba maeneo mbalimbali ya nchi hiyo.

Habari zaidi kutoka nchini Morocco zinaeleza kuwa idadi ya vifo inaweza kuongezeka kwa kuwa bado kuna idadi kubwa ya watu wamenasa kwenye vifusi huku zoezi la uokoaji likiendelea.

Kufuatia tetemeko hilo, Mfalme Mohammed VI wa Morocco ameagiza Jeshi la nchi hiyo kufanya kazi ya kuwaokoa watu waliokumbwa na tetemeko hilo na ametaka kazi hiyo ifanyike kwa kutumia helikopta pamoja na ndege zisizo na rubani.

Tetemeko hilo kubwa la ardhi lililoikumba Morocco limeharibu makazi ya maelfu ya raia wa nchi hiyo na miundombinu huku ikielezwa kuwa jiji maarufu la kibiashara la Marrakesh nalo limeharibiwa vibaya.