Umoja wa Mataifa wataka kuimarishwa demokrasia Afrika

0
197

Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Turk ametoa wito wa kurejeshwa haraka utawala wa kirai kwenye mataifa ya Afrika yalioshuhudia mapinduzi ya kijeshi.

Volker Turk amesema mwenendo wa kuchukua madaraka kwa nguvu sio suluhu kwa matatizo yaliyopo.

Pia, amesema njia pekee ya kuyashughulikia matatizo ni kuwa na utawala wa kiraia unaotoa nafasi kwa umma kuwa huru kuikosoa serikali na kushinikiza mageuzi.

Aidha, amezungumzia athari za mabadiliko ya tabianchi na ukosefu wa huduma muhimu, ndiyo yanachangia hali ya kukata tamaa miongoni mwa raia duniani na kuchochea hisia za itikadi kali.

Pia, Volker Turk aliongezea baadhi ya changamoto zinazoikumba dunia ni kama vile ukosefu wa usalama nchini Haiti na ukandamizaji wa makundi ya walio wachache ulimwenguni.