Mavunde atangaza vita na watorosha madini

0

Waziri wa Madini, Anthony Mavunde amesema kuwa ataweka mkazo mkubwa katika kudhibiti vitendo vya utoroshaji madini, ikiwa ni moja ya mikakati yake ya kukuza sekta hiyo, ili kuhakikisha kuwa rasilimali hiyo muhimu inauzwa katika mfumo rasmi ili iweze kuwanufaisha Watanzania wote.

Akizungumza katika mahojiano na kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC, Mavunde amesema sekta ya madini imeendelea kuonesha mwelekeo chanya, ikiwemo mchango wake kwenye uchumi, hivyo wamejipanga kuhakikisha kuwa malengo yaliyowekwa yanafikiwa.

Mbali na kudhibiti utoroshaji madini, amesema mkakati mwingine wanaouchukua kuongeza tija ni kuimarisha masoko na vituo vya kuuza madini ambayo yataongeza makusanyo ya sekta hiyo kufikia lengo la shilingi trilioni 1 katika mwaka 2023/24.

Aidha, amesema wachimbaji wadogo wana mchango mkubwa kwenye ukuaji wa sekta hiyo, akitolea mfano kuwa katika maduhuli ya shilingi bilioni 648 yaliyokusanywa mwaka 2022/23, zaidi ya asilimia 40 zilitoka kwa wachimbaji wadogo. Kutokana na mchango wao mkubwa, Serikali itaendelea kuwawezesha wafanye kazi zao kwa ufanisi zaidi, ambapo moja ya hatua inayochukuliwa ni kusajili wachimbaji wote nchini, ili kuwa na taarifa zao ikiwemo eneo walipo na shughuli wanayofanya.

Katika mwaka uliopita sekta hiyo ilichangia asilimia 15 ya makusanyo yote, asilimia 56 ya fedha za kigeni na ilikuwa na mchango wa asilimia 9.1 kwenye pato la Taifa ambapo lengo ni kufikia asilimia 10 ifikapo mwaka 2025.

The U.S. Ambassador applauds Dr. Biteko’s appointment.

0

Dr. Biteko promises cooperation with International Energy Sector Organizations.

Deputy Prime Minister and Minister of Energy, Dr. Doto Biteko, held a meeting and discussions with the U.S. Ambassador to Tanzania, Dr. Michael Battle, during his courtesy visit today, September 13, 2023, at the Ministry’s Sub Office in Dar es Salaam.

Dr. Battle visited Hon. Biteko with the aim of congratulating him on his appointment and new responsibilities, as well as discussing various issues of sectoral cooperation between the two countries.

During their discussions, Hon. Biteko stated that the Ministry will continue to collaborate with national and international stakeholders in the implementation of various energy sector projects, including those for electricity production and the liquefied natural gas (LNG) project.

Hon. Biteko mentioned that negotiations between the government and LNG project investors are progressing well, with experts reviewing the contract terms to ensure satisfaction on both sides. However, he hinted at the possibility of revising some terms to further improve them.

“We are continuing to review and improve certain aspects of this contract so that when it is ready, it can serve as a tool to ensure the expectations and benefits of this project are achieved,” explained Hon. Biteko.

Ambassador Battle also informed Hon. Biteko that there are two American companies, Astra Energy and Upepo Energy, with the intention to invest in Tanzania in the field of electricity production.

Addressing the issue, Hon. Biteko promised to expedite the matter, particularly given the current high demand for electricity in the country.

Moreover, Ambassador Battle expressed confidence that Hon. Biteko will excel in overseeing the Energy Sector, considering his extensive experience in the Extractive Industry, including the type of contracts he encountered during his tenure as the Minister of Minerals.

Jafo: Acheni kununua majokofu, viyoyozi vya mtumba

0

Serikali imewataka wananchi kuepuka kuingiza nchini na kutumia majokofu au viyoyozi vilivyokwishatumika (mtumba) ambavyo vinatumia gesi haribifu kwa tabaka la ozoni na badala yake watumie bidhaa zenye uwezo mdogo wa kuchangia ongezeko la joto duniani.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi Ya Makamu Wa Rais (Muungano Na Mazingira) Dkt. Selemani Jafo, wakati akitoa Tamko kuhusu Siku ya Kimataifa ya Hifadhi ya Tabaka la Ozoni jijini Dodoma.

Amesema hayo wakati Tanzania ikitarajia kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Hifadhi ya Tabaka la Ozoni, Septemba 16, 2023, kama kumbukumbu ya tarehe ya kutiwa saini Itifaki ya Montreal ya mwaka 1987 kuhusu kemikali zinazomong’onyoa Tabaka la Ozoni, ambalo kazi yake ni kuchuja sehemu kubwa ya mionzi ya jua isifike kwenye uso wa dunia.

Dkt. Jafo amesema tabaka la ozoni linapoharibiwa husababisha saratani ya ngozi, mtoto wa jicho, upungufu wa kinga dhidi ya maradhi, kujikunja kwa ngozi, kuathirika kwa ukuaji wa mimea pamoja na kuongezeka kwa joto duniani na hivyo kuchangia katika mabadiliko ya tabianchi.

Kauli mbiu ya Siku ya Kimataifa ya Hifadhi ya Tabaka la Ozoni mwaka huu ni “Hifadhi ya tabaka la ozoni na kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi,” ambayo imechaguliwa kutokana na mafanikio ya kimataifa kupitia utekelezaji wa Itifaki ya Montreal katika kuchangia jitihada za kuhifadhi tabaka la ozoni na kupunguza athari zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi.

UVCCM waandamana Mtwara kumpongeza Rais Samia

0

Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Mtwara wamempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji wa ilani ya chama hicho kwa vitendo.

Wakizungumza wakati wanakabidhi maandamano ya amani ya kumkaribisha Rais Samia kwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Ahmed Abbas wamesema ilani ya CCM kwa mkoa wa Mtwara imejenga miradi mbalimbali ya maendeleo.

Aidha, wameitaja baadhi ya miradi ya maendeleo iliyojengwa mkoani Mtwara na inayoendelea kujengwa ni kukamilika kwa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini, upanuzi wa Bandari ya Mtwara upanuzi wa kiwanja wa ndege.

Miradi mingine ni kuanza ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Mnivata- Tandahimba-Newala-Masasi ambapo wakandarasi wako site na uboreshaji wa miradi ya maji.

Akipokea maandamano hayo, Kanali Abbas amewataka wakazi wa Mtwara kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali za kuleta maendeleo pamoja na kuwataka kujitokeza kwa wingi kesho kwenye mapokezi ya Rais Samia anayetarajia kuanza ziara ya kikazi ya siku nne.

Serikali kuendelea kuajiri watumishi wa Afya nchini

0

Serikali itaendelea kuajiri watumishi wa Afya nchini kwa kuwa Rais Samia Suluhu Hassan anatoa kibali cha kuajiri watumishi wapya katika Sekta ya Afya kila Mwaka.

Hayo ameyasema Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alipokuwa akizungumza na watumishi wa Hospitali ya Wilaya ya Momba wakati akiendelea na ziara yake ya siku Tatu katika Mkoa huo.

“Tunamshukuru sana Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kujali Sekta ya Afya ambapo anatoa kibali kila Mwaka cha ajira mpya Kwa hiyo tutaendelea kuajiri lakini pia kutumia wadau wa maendeleo kuleta wataalamu hususan wa Maabara”. Amesema Waziri Ummy

Waziri Ummy amesema kufuatia changamoto hiyo ya uhaba wa watumishi katika Hospitali ya Wilaya ya Momba ni kutokana na kuongezeka kwa vituo vya Afya ambapo awali kulikua na vituo vya Afya Viwili na Sasa kuna Vituo vya Afya Vitano.

Aidha, Waziri Ummy amewataka watumishi wa Afya katika Hospitali ya Wilaya ya Momba kuhakikisha wanaendelea kufanya kazi kwa kufuata misingi ya Taaluma yao, weledi na maadili ili wananchi kuendelea kupata huduma bora.

“Muda wote tapohudumia wagonjwa tuzingatie weledi na Taaluma zetu na la pili tuzingatie maadili ya Taaluma yetu na la Tatu tuzingatie viapo vyetu kwa kuwa kazi yetu ni kuokoa maisha ya watu”. Amesema Waziri Ummy

Waziri Ummy Mwalimu yupo katika Mkoa wa Songwe kwa ziara ya siku Tatu kwa lengo la kukagua huduma zinazotolewa katika Hospitali a Wilaya, vituo vya Afya pamoja na Zahanati, pia upatikanaji wa dawa na utolewaji wa chanjo.

Rais Dkt. Mwinyi amwakilisha Rais Samia kwenye mkutano Cuba

0

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameondoka Zanzibar kuelekea Havana, Cuba, kumwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan, katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la 77 na China (G77+ China) utakaofanyika kuanzia tarehe 15 hadi 16 Septemba 2023.

Mkutano huo unalenga kukutanisha Mataifa yanayoendelea (Developing Countries) ili kujadili changamoto zinazoikabili dunia, hususan baada ya kuathiriwa na janga la UVIKO-19 na migogoro inayoendelea duniani, pamoja na vikwazo mbalimbali vya kiuchumi.

Hivyo, mkutano huo utajikita zaidi katika kutafuta njia bora za kujenga ustahimilivu kupitia maendeleo ya sayansi, teknolojia, na ubunifu ili kundi la G77 na China liweze kufikia malengo yake kwa pamoja.

Mkutano huu utaongozwa na kaulimbiu isemayo “Current Development Challenges: The Role of Science, Technology and Innovation.”

Rais Dkt. Mwinyi anatarajiwa kutoa hotuba katika mkutano huo na kuelezea vipaumbele vya Tanzania, pamoja na hatua zilizochukuliwa kukuza utafiti na kuimarisha matumizi ya sayansi, teknolojia, na ubunifu (STI) katika kuleta mapinduzi ya kiuchumi.