Rais ateua Katibu Mkuu, Naibu AG

0

Balozi Stephen Mbundi ameteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu Mkuu wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki atakayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki.

Balozi Mbundi anachukua nafasi ya Balozi Kennedy Gastorn ambaye ameteuliwa kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Rais Samia.Suluhu Hassan pia amemteua Balozi Said Shaib Mussa ambaye ni Balozi wa Tanzania huko Kuwait kuwa Naibu Katibu Mkuu wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Balozi Mussa anachukua nafasi ya Balozi Fatma Rajab ambaye ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania, Oman.

Balozi Kennedy Gastorn yeye ameteuliwa kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Balozi Gastorn anachukua nafasi ya Dkt. Evaristo Longopa ambaye ameteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kurugenzi ya Mawasiliano.ya Rais, Ikulu, uteuzi huo umeanza Septemba 03, 2023.

Rais Samia Ateua Majaji

0

Rais Samia Suluhu Hassan ameteua Majaji wanne wa Mahakama ya Rufani na Majaji Ishirini wa Mahakama Kuu, uteuzi ulioanza Septemba 03, 2023.

Majaji wa Mahakama ya Rufani walioteuliwa ni
Jaji Lameck Mlacha ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kigoma na Jaji Paul Ngwembe ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Morogoro.

Wengine walioteuliwa kuwa Majaji wa Mahakama.ya Rufani ni Mustafa Kambona Ismail ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Divisheni ya Rushwa na Uhujumu, Dar es Salaam na Jaji Abdul-Hakim Ameir Issa ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu, Zanzibar.

Majaji wa Mahakama Kuu walioteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan ni
Dkt. Evaristo Longopa ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Amemteua Wilbert Chuma kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Chuma alikuwa Msajili Mkuu wa Mahakama ya Rufani Dar es Salaam.

Amemteua Sharmillah Said Sarwat kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Sarwat alikuwa Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam.

Amemteua Arnold Kirekiano kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi Kirekiano alikuwa Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam.

Amemteua Martha Mpaze kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Mpaze alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama Jumuishi katika Masuala ya Mirathi na Familia, Dar es Salaam.

Amemteua Ferdinand Kiwonde kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Kiwonde alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu.

Amemteua Said Ding’ohi kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Ding’ohi alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Iringa.

Amemteua Dkt. Angelo Rumisha kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Dkt. Rumisha alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam.

Amemteua Sarah Mwaipopo kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo alikuwa Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam.

Amemteua Ntuli Mwakahesya kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Mwakahesya alikuwa Naibu Karani wa Baraza la Mawaziri, Ofisi ya Rais Ikulu, Dodoma.

Amemteua Griffin Mwakapeje kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Mwakapeje alikuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria, Wizara ya Katiba na Sheria, Dodoma.

Amemteua Dkt. Dafina Ndumbaro kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Dkt. Ndumbaro alikuwa Wakili wa Serikali Mwandamizi, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dodoma.
Amemteua Emmanuel Kawishe kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Kawishe alikuwa Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Dodoma.

Amemteua Abdallah Halfan Gonzi kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Gonzi alikuwa Mjumbe wa Baraza la Rufani za Kodi (TRAT) na Mhadhiri Msaidizi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Amemteua Kamazima Kafanabo Idd kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi Idd alikuwa Mhadhiri Msaidizi Chuo cha usimamizi wa Fedha (IFM), Dar es Salaam.

Amemteua Frank Mirindo kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Mirindo alikuwa Mhadhiri Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA), Tanga.

Amemteua Hadija Kinyaka kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Kinyaka alikuwa Wakili wa Kujitegemea Kampuni ya Uwakili ya Lawhill Co. & Advocates, Dar es Salaam.

Amemteua Aisha Ally Sinda kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi Sinda alikuwa Wakili wa Kujitegemea Kampuni ya Uwakili BOWMANS Tanzania, Dar es Salaam.

Amemteua Hussein Salum Mtembwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Mtembwa alikuwa Wakili wa Kujitegemea na Mmiliki wa Kampuni ya Uwakili ya HM Noble Attorneys, Mtwara.

Amemteua Irene Musokwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Musokwa alikuwa Wakili wa Kujitegemea na Mshiriki katika Kampuni ya Uwakili ya FC Attorneys, Dar es Salaam.

Kilimo cha Karafuu Zanzibar kuboreshwa

0

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea na mikakati yake ya kuboresha kilimo cha Karafuu ambacho kimeipatia Zanzibar umaarufu mkubwa.

Kauli iiyo imetolewa mkoani Dar es Salaam na Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar Shamata Shaame Khamis
wakati wa mkutano wa Wahariri wa vyombo vya Habari ulioandaliwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu kuelekea mkutano wa Mifumo ya Chakula Afrika 2023 utakaofanyika Septemba 05,2023 hadi Septemba 08, 2023 nchini Tanzania.

Amesema Zanzibar imeweka nguvu kubwa katika kuendeleza zao la Karafuu kutokana na umuhimu wake Visiwani humo sio tu kwa sekta ya kilimo pekee bali pia kwa sekta ya Utalii.

Waziri Shamata amesema kwa sasa Zanzibar inajivunia kuzalisha Karafuu yenye ubora zaidi ambayo inahitajika katika maeneo mbalimbali duniani.

Kuhusu sekta ya Kilimo Zanzibar, Waziri Shamata amesema inachangia kwa Asilimia 22 katika Pato la Zanzibar.

Ni Simba vs Al Ahly African Football League

0

Simba SC itafungua pazia la African Football League kwa kucheza dhidi ya Al Ahly ya Misri.

Michezo mingine TP Mazembe itakutana na Esperance Sportive De Tunis, Enyimba DC itacheza na Wydad AC huku Atletico Petroleos De Luanda ikikutana na Mamelodi Sundowns FC.

Mashindano hayo yataanzaa Oktoba 20, 2023 jijini Dar es Salaam na yanatarajiwa kufikia tamati Novemba 11 mwaka huu.

Michezo yote kwenye mashindano haya itakuwa nyumbani na ugenini.

TFF: Waziri Dkt. Ndumbaro hajafungiwa

0

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limesema kuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro alishinda rufaa ya adhabu ya kufungiwa miaka saba iliyotolewa na uongozi wa TFF uliopita.

Ufafanuzi wa TFF umekuja kufuatia uwepo wa taarifa ya kuwa Dkt. Ndumbaro alifungiwa tangu mwaka 2017.

Kamati ya Rufani ya Nidhamu ya TFF chini ya uongozi wa sasa ilisikiliza rufani hiyo mwaka 2017 ambapo Waziri Dkt. Ndumbaro alishinda, hivyo kuondolewa adhabu ya kufungiwa,”- imesema taarifa ya TFF.

TFF imeongeza kuwa Dkt. Ndumbaro ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani ya Leseni za klabu ya TFF.

Mtanzania asajiliwa Shakhtar Donetsk inayoshiriki UEFA

0

Shakhtar Donetsk ya Ukraine imemsajili kwa mkopo kiungo wa kimataifa wa Tanzania, Novatus Dismas akitokea Zulte Waregem ya nchini Ubelgiji.

Novatus alitambulika kwenye soka la kulipwa akiwa Azam FC ambapo baadaye alisajiliwa Maccabi ya nchini Israel mwaka 2020.

Msimu wa 2021/22 alicheza kwa mkopo Beitar Tel Aviv ya Israel na majira ya joto mwaka 2022 alijiunga na Zulte kwa mkataba wa miaka mitatu.

Shakhtar Donetsk inashiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya ambapo imepangwa kundi moja pamoja na FB Barcelona, FC Porto na Royal Antwerp F.C.

Kinda huyo wa Kitanzania alizaliwa Septemba 2, 2002, na alichezea timu ya Taifa mchezo wake wa kwanza Septemba 2, 2021.