Man U yapigania ubingwa

0

Kocha wa muda wa timu ya Manchester United, – Ole Gunner  Solskjaer amesema kuwa timu yake haipiganii kumaliza ligi ikiwa kwenye Top 4 bali inapigania ubingwa.

Kwa sasa Manchester United ni ya sita kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England na bado iko kwenye michuano ya ligi ya mabingwa Barani Ulaya na kombe la FA ambapo watapambana na Chelsea kwenye mzunguko wa tano.

Ole Gunnar Solskjaer aliyechezea Manchester United kwa muda wa  miaka  11 amesema kuwa, siku zote timu hiyo ni ya kuwania mataji na sio ya kupigania kuingia kwenye Top 4.

Jeuri ya kocha huyo inakuja baada ya kushinda michezo yake yote sita aliyoiongoza timu hiyo tangu achukue jukumu hilo toka kwa Jose Mourihno.

Pamoja na maneno hayo ya kujiamini ya Ole Gunnar, lakini timu yake iko nyuma kwa pointi 16 dhidi ya vinara Liverpool, na ina tofauti ya pointi nne tu kutinga kwenye Top 4.

Majaji watakiwa kuzingatia sheria

0

Rais  John Magufuli amewaapisha Majaji wa Mahakama ya Rufani na wengine wa Mahakama Kuu aliowateua hivi karibuni na kusema kuwa kazi ya kusimamia haki ina changamoto kubwa, hivyo majaji hao wanatakiwa wamtangulize Mwenyezi Mungu katika kutekeleza majukumu yao.

Wakati wa hafla hiyo iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es salaam, Rais Magufuli pia ameshauri Majaji hao wapya kuzingatia sheria pamoja na katiba ya nchi katika utendaji kazi wao wa kila siku  hasa katika kuwahudumia Watanzania ambao  wengi wao wamekua walikosa haki yao ya kisheria.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli, ataendelea kuteua Majaji wengi zaidi  kadri bajeti itakavyoruhusu kwa kuwa bado mahitaji ya Majaji hao ni makubwa.

Kwa upande wa Wakuu wapya wa wilaya za Tarime mkoani Mara na Mwanga mkoani Kilimanjaro ambao nao amewateua hivi karibuni pamoja na Wakuu wengine wa wilaya nchini, Rais  Magufuli amewaagiza kutotumia madaraka yao vibaya na kuacha tabia ya  kuwaweka watu ndani pasipo kuzingatia utaratibu kama inavyofanywa hivi sasa na baadhi yao.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan alipata fursa ya kuzungumza wakati wa hafla hiyo,  ambapo Majaji Sita wa Mahakama ya Rufani na wengine  Kumi na Watano wa Mahakama Kuu wameapishwa, huku wakuu wa wilaya mawili na Wakurugenzi Kumi wa halmashauri za wilaya wamepatiwa maelekezo ya kikazi na kula kiapo cha uadilifu kwa viongozi wa umma.

Akizungumza na watendaji hao, Makamu wa Rais ameelezea furaha yake kutokana na ongezeko la Majaji wanawake na kuwataka kufanya kazi huku wakiyatazama kwa ukaribu makundi mbalimbali ambayo yamekua yakilalamika kukosa haki.

Naye Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa  Ibrahim Juma ametoa  wito kwa majaji hao  wapya  kufanya kazi kwa kujituma na kwa haraka ili kuweza kushughulikia mashauri mengi zaidi.

Ameelezea matumaini yake kuwa Majaji hao wapya watatenda haki na kutoruhusu malalamiko ya aina yoyote.

Majaji wa Mahakama ya Rufani walioapishwa katika hafla hiyo ni Sahel Barke, Jaji Mary Levira, Jaji Rehema Sameji,  Jaji Winnie Korosso, Jaji Ignus Kitusi na Jaji Lugano Mwandambo.

Majaji walioapishwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ni pamoja na Cyprian Mkeha, Jaji Dunstan Ndunguru, Jaji Mwinshehe Kulita, Jaji  Ntemi Kilikamajenga,  Jaji Zepherine Galeba na Jaji Juliana Masabo.

Majaji wengine walioapishwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ni Mustapha Ismail,  Jaji Upendo Madeha,  Jaji Willbard Mashauri,  Jaji Yohane Masara,  Jaji Lilian Mongella,  Jaji Fahamu Mtulya,  Jaji John Kahyoza, Jaji Athumani  Kirati na Jaji Susan Mkapa.

Wakurugenzi wa halmashauri za wilaya walioteuliwa ili kujaza nafasi zilizokuwa wazi ni pamoja na Isaya Mbenje anayekwenda halmashauri ya  Pangani, Dkt Fatuma Mganga halmashauri ya  Bahi, Regina Bieda, -Tunduma, Jonas Mallosa halmashauri ya Ulanga, Ally Juma Ally anayekwenda Njombe  na  Misana Kwangura halmashauri ya Nkasi.

Wengine ni Diodes Rutema halmashauri ya Kibondo, Netho Ndilito halmashauri ya Mufindi, Elizabeth Gumbo halmashauri ya Itilima na Stephen Ndaki anayekwenda halmashauri ya Kishapu.

Wakuu wapya wa wilaya ni Charles Kabeho aliyeteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Tarime mkoani Mara na Thomas Apson ambaye anakua mkuu wa wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro.

Viongozi walioteuliwa karibuni waapishwa

0

Rais John Magufuli amewaapisha Majaji Sita wa Mahakama ya Rufani na Majaji Kumi na Watano wa Mahakama Kuu aliowateua hivi karibuni.

Majaji wa Mahakama ya Rufani walioapishwa katika hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam ni Sahel Barke, Jaji Mary Levira, Jaji Rehema Sameji,  Jaji Winnie Korosso, Jaji Ignus Kitusi na Jaji Lugano Mwandambo.

Majaji walioapishwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ni pamoja na Cyprian Mkeha, Jaji Dunstan Ndunguru, Jaji Mwinshehe Kulita, Jaji  Ntemi Kilikamajenga,  Jaji Zepherine Galeba na Jaji Juliana Masabo.

Majaji wengine walioapishwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ni Mustapha Ismail,  Jaji Upendo Madeha,  Jaji Willbard Mashauri,  Jaji Yohane Masara,  Jaji Lilian Mongella,  Jaji Fahamu Mtulya,  Jaji John Kahyoza, Jaji Athumani  Kirati na Jaji Susan Mkapa.

Katika hafla hiyo,  wakuu wa wilaya mawili na Wakurugenzi Kumi wa halmashauri za wilaya ambao pia waliteuliwa na Rais Magufuli Januari 27 mwaka huu, nao wamepatiwa maelekezo ya kikazi na kula kiapo cha uadilifu kwa viongozi wa umma.

Wakurugenzi hao wa halmashauri za wilaya walioteuliwa ili kujaza nafasi zilizokuwa wazi ni pamoja na Isaya Mbenje anayekwenda halmashauri ya  Pangani, Dkt Fatuma Mganga halmashauri ya  Bahi, Regina Bieda, -Tunduma, Jonas Mallosa halmashauri ya Ulanga, Ally Juma Ally anayekwenda Njombe  na  Misana Kwangura halmashauri ya Nkasi.

Wengine ni Diodes Rutema halmashauri ya Kibondo, Netho Ndilito halmashauri ya Mufindi, Elizabeth Gumbo halmashauri ya Itilima na Stephen Ndaki anayekwenda halmashauri ya Kishapu.

Wakuu wapya wa wilaya ambao nao wamepatiwa maelekezo ya kikazi na kula kiapo cha uadilifu kwa viongozi wa umma Ikulu jijini Dar es salaam ni Charles Kabeho aliyeteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Tarime mkoani Mara na Thomas Apson ambaye anakua mkuu wa wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro.

Mtolea aapishwa

0

Mkutano wa 14 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umeanza jijini Dodoma.

Mkutano huo umeanza kwa kuapishwa kwa Mbunge mteule wa jimbo la Temeke mkoani Dar es salaam kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdallah Mtolea.

Mtolea alitangazwa kupita bila kupingwa mwezi Disemba mwaka 2018 baada ya Novemba 15 mwaka huohuo wa 2018 kutangaza Bungeni jijini Dodoma kukihama Chama Cha Wananchi (CUF) na kuhamia CCM.

Baada ya kiapo hicho Spika wa Bunge, -Job Ndugai alitoa taarifa kwa Bunge kuhusu kusainiwa kwa Muswada wa Sheria Ndogo za Fedha wa mwaka 2018, na hivyo kuwa sheria kamili.

Serikali yaboresha huduma kwa watu wenye ulemavu

0

Serikali ya imeweka mipango madhubuti ya kuboresha huduma na mazingira katika makundi mbalimbali ya watu wenye ulemavu.

Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es salaam  na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana na Ajira, -Anthony Mavunde kwa niaba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati wa uzinduzi wa Taasisi ya Haji Manara Foundation  na kuongeza kuwa serikali imeweka mipango ya kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata fursa sawa katika masuala ya kisiasa,kijamii na ushiriki katika ustawi na ujenzi wa Taifa.

Naibu Waziri Mavunde amempongeza  Haji Manara kwa uamuzi na utayari katika kusaidia watu wenye Ualbino na kwamba serikali itatoa kila ushirikiano kwa Taasisi hiyo katika kutimiza majukumu yake hasa katika kutoa elimu kwa jamii juu ya nafasi ya watu wa kundi hilo.

Kwa upande wake Haji Manara amesema  kuwa Taasisi hiyo itasaidia kuwajengea uwezo watu wenyeUalbino pamoja na kutoa elimu kwa jamii juu ya kuepukana na dhana potofu juu ya watu hao.

Naye mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, -Paul Makonda  ametumia uzinduzi huo Taasisi ya Haji Manara Foundation  kumpongeza Haji Manara kwa ubunifu na kuitaka jamii kuwaunga mkono watu wanaoleta mabadiliko na fikra mpya na sio kuwavunja moyo kwa maneno yasiyofaa.

Watuhumiwa wa ujambazi wauawa Kigoma

0

Watu wanane wanaotuhumiwa kuwa ni majambazi wameuawa katika majibizano ya risasi na askari wa Jeshi la polisi mkoani Kigoma kwenye pori la Muyovozi wilayani Kakonko.

 Kamanda wa polisi wa mkoa wa Kigoma, – Martin Ottieno amesema kuwa jeshi hilo lilipata taarifa kutoka kwa Wakazi wa kijiji cha  Mganza kuhusu uwepo wa vibarua wa mashambani wanaowatilia mashaka na walipokua wakiwafuatilia ndipo watu hao walipoanza kurusha risasi.

Kamanda Ottieno  ameongeza kuwa katika tukio hilo, mbali na kuuawa kwa watuhumiwa hao wa ujambazi, polisi pia wamekamata bunduki moja aina ya AK 47 ikiwa na risasi Kumi.

Idadi ya waliokufa Brazil yaongezeka

0

Idadi ya watu waliokufa baada ya kuvunjika kwa kingo za bwawa moja la maji lililopo kwenye mgodi mkubwa wa chuma wa Vale nchini Brazil imeongezeka na kufikia 58.

Watu wengine zaidi ya mia tatu, wengi wao wakiwa wafanyakazi wa mgodi huo uliopo kwenye jimbo la Minas Gerais  Kusini Mashariki mwa Brazil hawajulikani walipo.

Mpaka sasa vikosi vya uokoaji nchini Brazil ambavyo vimekua vikitumia helikopta 13,  vimeshindwa kuwapata watu ambao awali walidhaniwa kuwa wako hai.

Kwa mujibu wa idara ya Zimamoto nchini Brazil,  takribani watu elfu 24 wamehamishwa kutoka kwenye nyumba zao zilizopo katika maeneo  mbalimbali ya jimbo hilo la Minas Gerais kufuatia kuwepo kwa wasiwasi wa kutokea kwa madhara zaidi.

Barcelona tishio LA LIGA

0

Timu ya FC Barcelona imeendelea kuwa tishio katika ligi soka daraja la kwanza nchini Hispania (LA LIGA),  baada ya kuitandika timu ya Girona mabao mawili kwa bila.

Mabao  ya wachezaji Nelson Semedo katika dakika ya Tisa na la Lionel Messi kwenye dakika ya 68 ndiyo yamepeleka kilio kwa Girona na kupoteza alama Tatu muhimu .

Messi sasa amefikisha mabao 26 msimu huu na kuisaidia timu yake ya FC Barcelona kufikisha alama 49 kileleni mwa msimamo wa LA LIGA.

Nao wapinzani wa wa jadi wa FC Barcelona timu ya  Real Madrid wakiwa ugenini,  wamepata ushindi mnono baada ya kuwanyuka Espanyol mabao manne kwa mawili.

Mabao ya Karim Benzema aliyefunga mabao mawili, Sergio Ramos na Gareth Bale waliofunga bao moja kila mmoja ndio yamewapa ushidi huo mnono Real Madrid na kufikisha alama 39 wakiwa katika nafasi ya Tatu kwenye msimamo wa LA LIGA.