Waziri Mkuu kuongoza mazishi ya Dkt Mengi

0
408

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuongoza mazishi ya Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, –  Dkt Reginald Mengi yatakayofanyika kesho  Alhamisi Mei  Tisa  kijijini kwake Kisereni, Machame wilayani Hai mkoani  Kilimanjaro.

Waziri Mkuu ataongoza mazishi hayo kwa niaba ya Serikali ambapo Ibada ya mazishi itafanyika kwenye Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) la Kisereni, Machame.

Tayari mwili wa Dkt Mengi ambaye alifariki dunia Mei 2 mwaka huu huko Dubai, umewasili mkoani Kilimanjaro ukitokea jijini Dar es salaam na kupokelewa na mamia ya wakazi wa mkoa huo.