Waziri Mkuu amefika katika shule ya Msingi Mwisenge aliyosoma Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kujionea ukarabati wa kisasa uliofanyika katika Shule hiyo ikiwa ni kutunza kumbukumbu muhimu katika shule hiyo
Waziri Majaliwa ameitaka Halmashauri ya Manispaa ya Musoma kuhakikisha wanatunza Shule hiyo sambamba na kufanya marekebisho madogo madogo yanayojitokeza
