Wakulima Zanzibar wasisitizwa kilimo cha mbogamboga

0
873

Waziri asiyekuwa na Wizara maalum Juma Ali Khatib amewataka wakulima wa visiwa vya Zanzibar kuhakikisha wanajikita katika sekta ya kilimo cha mboga mboga, matunda na viungo ili kupunguza utegemezi wa bidhaa hizo kutoka nje ya visiwa hivyo.

Akizungumza mjini Unguja wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi wa jengo la kutoa mafunzo ya kilimo biashara Waziri Khatib amesema umefika wakati kwa wakulima kujikita katika mapinduzi ya kilimo kwa kutumia teknolojia ya kisasa na kufuata ushauri wa wataalum wa kilimo.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Ahmad Kassim Haji amewataka vijana kuzitumia vizuri fursa za kilimo na kujiunga na jumuiya zinazoelimisha wakulima ili wajiajiri.