Upanuzi wa bandari ya Kagunga mkoani Kigoma umefikia hatua nzuri

0
1478

Mamlaka ya usimamizi wa bandari Tanzania   TPA imesema ipo katika hatua za mwisho  za kuanza awamu ya pili ya ujenzi na upanuzi wa bandari ya Kagunga iliyopo kaskazini mwa ziwa Tanganyika  mkoani  Kigoma.

Mkurugenzi mkuu wa Tpa mhandisi Deusdedit Kakoko upanuzi huo wa bandari ya Kagunga utasaidia kurahisisha  biashara kwa nchi za mwambao wa ziwa Tanganyika na kudhibiti mianya ya utoroshaji wa bidhaa.

Amesema kuwa kazi hiyo  ambayo  pia itahusisha na  uendelezaji wa ujenzi wa  soko la  ujirani mwema Kagunga  itaanza mwanzoni  mwa mwezi janury mwaka 2019.

Tayari gati na majengo ya kisasa vimekamilika, ishara ya kuelekea hatua za mwisho za ujenzi wa bandari hii inayoelezwa kuwa ya kipekee kutokana na kuwa na eneo kubwa lenye kina cha maji cha kutosha kwa ajili ya kuhudumia meli.