Mamlaka ya Usafiri wa Anga Nchini – TCAA imesema inashughulikia maombi ya kampuni ya ndege ya Fastjet kuingiza ndege nchini kwakuwa lengo la mamlaka hiyo ni kuhakikisha huduma za usafiri wa anga zinakuwa salama kwa wateja wake.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Hamza Johari amesema Mamlaka hiyo haijazuia Fastjet kuingiza ndege mpya kwa ajili ya kuendelea na biashara nchini.
Johari amesema mamlaka hiyo inapenda kuona huduma ya usafiri wa anga inakuwa na ushindani na kutoa huduma zenye uhakika na usalama kwa wateja wake.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi za sekta binafsi Godfrey Simbeye amezishauri taasisi binafsi kuzingatia sheria katika uendeshaji wa shughuli zao.
