Facebook Instagram Twitter Youtube
  • Home
  • Kuhusu TBC
    • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
    • Privacy Policy
  • Kitaifa
  • Kimataifa
  • Michezo
  • Burudani
  • Biashara
  • Tuzo
  • Live Stream
    • TBC1
    • TBC2
Search
. .
  • Home
  • Kuhusu TBC
    • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
    • Privacy Policy
  • Kitaifa
  • Kimataifa
  • Michezo
  • Burudani
  • Biashara
  • Tuzo
  • Live Stream
    • TBC1
    • TBC2
Home Kitaifa Serikali yawaahidi makubwa wakandarasi wazawa
  • Kitaifa

Serikali yawaahidi makubwa wakandarasi wazawa

By
Dickson Mushi
-
May 13, 2022
0
207
Share
Facebook
Twitter
WhatsApp
Linkedin

    Serikali imeahidi kutenga fedha kwa ajili ya kuwapa miradi ya ujenzi makandarasi wazalendo ikiwa ni sehemu ya kuwajengea uwezo kutekeleza miradi mikubwa huku ikiwataka wawe waaminifu.

    Ahadi hiyo imetolewa na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Pof. Makame Mbarawa, wakati akifungua mkutano wa mashauriano kwa makandarasi wa ndani unaoendelea mkoani Dodoma.

    “Nitamuomba Rais Samia suluhu Hassan atoe fedha kwa miradi mikubwa itakayotekelezwa lakini mkipewa kazi naomba muwe na bei halisi ambazo hazitatutisha na tunataka kuona thamani ya fedha ili tuone umuhimu wa kuwapa miradi,” alisema

    Waziri Mbarawa amesema makandarasi wanawajibu wa kuinua uchumi wa nchi hivyo wanapaswa kutambua jukumu hilo wanapopewa miradi kwani wakichelewesha au kufanya chini ya kiwango wanakwamisha maendeleo ya nchi na kuwakosesha wananchi haki ya kutumia miradi hiyo kwa wakati.

    “Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB) mmezungumzia Force account sasa nawaagiza tumieni wataalamu wenu kufanya utafiti kama sababu zilizoifanya serikali kutumia utaratibu huo zipo au hazipo, serikali ya awamu ya sita ni sikivu na kama hakuna haja ya kutumia utaratibu huo tutawapa kazi nyingi ila muwe waaminifu,” alisema

    Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya CRB, Consolata Ngimbwa aliiomba serikali kuachana na utaratibu wa Force Account na kuwapa makandarasi wa ndani kufanya miradi hiyo kwani wengi wao kwa kukosa kazi wako kwenye hali mbaya.

    Alisema makandarasi wa fani ya ujenzi waliosajiliwa na bodi wako zaidi ya 4,000 na wamiliki wake wameathirika wao na wategemezi wao kwa kiwango kikubwa kutokana na kukosa kazi kwa muda mrefu na wengine wameshakata tamaa.

    • TAGS
    • Force Account
    • MAKAME MBARAWA
    • wakandarasi
    • WAziri wa Ujeezi
    Facebook
    Twitter
    WhatsApp
    Linkedin
      Previous articleMaofisa habari wapewa somo
      Next articleVituo vya Afya kupata vifaa tiba kabla ya Oktoba
      Dickson Mushi
      http://www.tbc.go.tz
      Facebook Instagram Twitter
      Sign in
      Welcome! Log into your account
      Forgot your password? Get help
      Password recovery
      Recover your password
      A password will be e-mailed to you.
      © Newspaper WordPress Theme by TagDiv
      Skip to toolbar
      • About WordPress
        • WordPress.org
        • Documentation
        • Support
        • Feedback
      • Log In