Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu SSRA

0
1282

Rais Dkt. John Magufuli leo tarehe 28 Desemba, 2018 ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii -SSRA Dkt. Irene Isaka.

Taarifa iliyotolewa na Ikulu imesema uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa SSRA utafanywa baadaye.

Dkt. Irene Isaka atapangiwa kazi nyingine.