Rais Dkt. John Magufuli leo tarehe 28 Desemba, 2018 ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii -SSRA Dkt. Irene Isaka.
Taarifa iliyotolewa na Ikulu imesema uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa SSRA utafanywa baadaye.
Dkt. Irene Isaka atapangiwa kazi nyingine.
