Rais kukutana na viongozi wa vyama vya wafanyakazi na watendaji wa mifuko nchini

0
1354

Rais. Dkt. John Magufuli anakutana na viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi –TUCTA, vyama shiriki, watendaji wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii –PSSSF na NSSF na Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii –SSRA, kujadili masuala yahusuyo mafao ya wafanyakazi hususani Kikokotoo.

Mkutano huo utafanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam ambapo Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Wizara husika watashiriki.

Mazungumzo ya Rais Magufuli na viongozi hao yatarushwa moja kwa moja yaani Live   na vyombo vya habari vya Redio, Televisheni, www.ikulu.go.tz, youtube ya ikulumawasiliano na mitandao ya kijamii muda wowote kunzia sasa