Baadhi ya wakazi wa jiji la DSM wametoa wito kwa wananchi jijini humo kujitokeza kwa wingi katika kupiga kura ya kuwachagua viongozi wa serikali za mitaa katika uchaguzi unaofanyika leo Nov 24 nchini Tanzania
Wakazi hao wamesema uchaguzi huo una umuhimu mkubwa kwa maendeleo ya jamii na taifa kwa jumla kwa kuwa viongozi wa mtaa wana mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi.
