Mkataba wa ujenzi wa mradi wa kufua umeme wa maji katika maporomoko ya mto Rufiji unasainiwa hii leo Ikulu jijini Dar Es Salaam.
Kabla ya utiaji saini mkataba huo viongozi wa dini mbalimbali akiwemo Askofu Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Mwingira wa Kanisa la Epatha, Sheikh Mohamed Rafik Turki wamefanya sala.
Mkandarasi kutoka nchini Misri anatarajiwa kujenga mradi huo.
Hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi huo imehudhuriwa na Rais Dkt. John Magufuli, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan,Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Misri Dkt. Mostafa Madbouly na viongozi wengine mbalimbali.
