Kyela kudhibiti utoroshaji wa kokoa

0
1256

Halmashauri  ya  wilaya  ya Kyela  mkoani  Mbeya  imesema kuwa   itaendelea  kudhibiti  utoroshaji  wa  kokoa katika halmashauri hiyo ili  kuongeza mapato.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti  wa  halmashauri  ya wilaya ya Kyela Dkt Hunter Mwakifuna mara  baada  kumalizika kwa kikao  cha  Baraza  la  Madiwani  la halmashauri hiyo kilichokua kikijadili mapendekezo ya bajeti  kwa mwaka wa fedha wa 2019/2020 .

Dkt Mwakifuna amesema kuwa tangu utoroshwaji huo wa kokoa kwenda nje ya wilaya hiyo Kyela kuanza kudhibitiwa mwaka 2017, mapato ya halmashauri hiyo yameongezeka kwa asilimia 90 hadi kufikia hivi sasa.

Kufuatia utoroshaji huo wa kokoa wilayani Kyela, Dkt Mwakifuna ametoa wito kwa wakulima wa zao hilo wilayani humo kuuza kokoa yao katika vyama vya ushirika, hatua ambayo pamoja na mambo mengine itasaidia kuongeza mapato ya halmashauri ya wilaya hiyo.