Kamanda Muslim awataka madereva kusitisha mgomo

0
526

Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani nchini FORTUNATUS MUSLIM amewataka madereva wa mabasi yaendayo mikoani kusitisha  mgomo uliotarajiwa kufanyika hapo kesho  na badala yake wafanye kazi  yao kama kawaida.

Kamanda MUSLIM  ameyasema hayo jijini DSM katika mkutano na waandishi wa habari na kuongeza  kuwa taarifa za mgomo huo wamezipata na kuzifanyia kazi na kwa kuwa suala hilo tayari  limefikishwa Mahakamani hivyo ni vyema madereva waache mahakama itoe maamuzi.