Jeshi la Polisi lapatiwa jengo Dodoma

0
180

Rais John Magufuli amelipatia Jeshi la Polisi nchini jengo la Ghorofa Nne lililopo jijini Dodoma, ambalo litatumika kama Makao Makuu ya Jeshi la Polisi nchini.

https://www.youtube.com/watch?v=szNFatTrqpI&feature=youtu.be

Akizungumza mara baada ya kuweka  jiwe la msingi la ujenzi wa  nyumba 118 za askari  zilizopo eneo la Nzuguni mkoani Dodoma, Rais Magufuli amesema kuwa, ameamua kutoa jengo hilo lilolokuwa mali ya  Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini  Dodoma (DUWASA) kwa kutambua kazi nzuri inayofanywa na Jeshi hilo.