Familia zatakiwa kuheshimu haki za watumishi wa ndani

0
828

Jamii imetakiwa kuwathamini na kuheshimu haki na mikataba ya watumishi wa ndani ili kumaliza mitafaruku inayotokea mara kwa mara ikiwemo unyanyasaji wanaofanyiwa watoto katika familia.

Ushauri huo umetolewa na Mwandishi wa kitabu cha Thamani ya Dada wa kazi za nyumbani, Astelia Bulugu na Mwalimu wa masuala ya malezi Wilbroad Prosper katika kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa na TBC One kwamba familia zinapaswa kuwaheshimu  wafanyakazi wa ndani kwani ni watu muhimu.

Aidha wadau hao wa masuala ya malezi wamesema wafanyakazi wa ndani ni kiungo muhimu katika familia hivyo wanatakiwa kupewa elimu mara kwa mara juu ya malezi, haki na wajibu wao.

Kukosekana kwa maelewano mazuri kati ya wazazi na watumishi wao wa ndani kumepelekea kutokea kwa matukio mbalimbali ya unyanyasaji unaofanywa na pande zote mbili huku baadhi ya matukio hayo yamepelekea vifo.