Afisa misitu asimamishwa kazi kwa tuhuma za kupiga wanawake.

0
1605

Naibu waziri wa maliasili na utalii Constantine Kanyasu ameagiza kusimamishwa kazi pamoja na kuchukuliwa hatua afisa nyuki wa hifadhi ya msitu wa kisiwa cha kome wilayani sengerema mkoani mwanza Gerald Athanas anayetuhumiwa kuwapiga wanawake wanaokwenda kuokota  kuni kwenye hifadhi hiyo.

Kanyasu ametoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko ya wananchi dhidi ya afisa huyo ambapo pia ametangaza kuondoa zuio linalokataza makambi ya uvuvi yaliyoko ndani ya  hifadhi hiyo kuezekwa kwa mabati.

Wavuvi walioko ndani ya hifadhi ya kisiwa cha kome kilichoko kwenye ziwa victoria wilayani sengerema mkoani mwanza wanatarajia kuondokana na tatizo la makambi yao kuteketea kwa moto mara kwa mara baada ya serikali kuruhusu wavuvi kuezeka makambi yao kwa kutumia mabati.

Kero nyingine iliyowasilishwa kwa naibu waziri Kanyasu ni wanawake kutoruhusiwa kunyonyesha watoto pamoja na kukatazwa kusenya kuni kwenye hifadhi msitu wa kisiwa cha kome.

Naye kaimu meneja wa wakala wa huduma za misitu-Tfs kanda ziwa Thomas Moshi amesema kitendo cha baadhi ya watumishi kujichukulia sheria mkononi hakikubaliki na kuwaasa watumishi wengine kuacha mara moja.