UTAFITI WA AWALI WAONYESHA MMEA WA MHAROBAINI UNAWEZA KUDHIBITI VIWAVI JESHI VAMIZI

0
341

Viwavi  jeshi  vamizi na mbegu zisizo stahimili magonjwa  na hali ya hewa  ni baadhi ya  changamoto kubwa  zinazoendelea  kuumiza  vichwa vya wataaalumu  nchini ilikutafuta  njia   bora ya kukabiliana na tatizo hilo .

Utafiti wa awali uliofanywa na wataalamu na watafiti wa chuo kikuuu cha sokoine cha kilimo sua morogoro umebaini  mmea wa muarobaini na mlonge unaweza kudhibiti viwavi jeshi vamizi katika mazao ikiwemo mahindi.

Mhadhiri wa chuo kikuu kutoka SUA ,Dr  Newton Kilasi amesema kukamilika kwa utafiti huo kutawezesha wakulima wengi zaidi kutumia mimea hiyo na kuachana kutumia  viuatilifu vyenye madhara kwa mazao  na ardhi.

Vilevile Dr Newton  Kilasi anaeleza namna walivyoamua kushirikiana na shirika la kilimo endelevu SAT kufanya tafiti zitakazo wasaidia wakulima wadogo wadogo  kukabiliana na tatizo hilo huku mtafiti  Martha Agustino akieleza  utafiti huo unavyoendelea kufanyika

Baadhi ya wakulima walitembelea  vitalu  vya utafiti kwa lengo la kujionea matumizi ya mimea hiyo wakaeleza namna  wanavyokabilina na viwavi jeshi vamizi sambamba na mwezeshaji kutoka shirika la SAT Elizabeth Girangai akilezea matarajio yao.