Wamiliki wa maeneo yaliyochukuliwa na Jeshi kuendelea kulipwa

0
448

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa  Dkt Hussein Mwinyi amesema kuwa serikali imetenga kiasi cha Shilingi Bilioni 19 kwa ajili ya kuwalipa wananchi waliochukuliwa  maeneo yao na Jeshi.

Akijibu swali Bungeni jijini Dodoma, Dkt Mwinyi amesema kuwa fedha hizo ambazo zilitengwa katika mwaka wa fedha wa 2018/2019 na zitaendelea kutolipwa mpaka madai hayo yatakapomalizika.

wananchi ambao wanadai kulipwa fidia ya maeneo yao.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Nishati  Subira  Mgalu  amesema kuwa serikali inaendelea na mchakato wa kusambaza nishati ya gesi asilia katika  maeneo mbalimbali nchini yakiwemo yale ya vijijini.

Bunge linaendelea na vikao vyake jijini Dodoma  ambapo Wabunge wanajadili bajeti ya wizara ya Viwanda na Biashara  kwa mwaka wa fedha  wa 2019/2020.