Rais Magufuli amjulia hali Dkt. Salim

0
1263

Rais Dkt. John Magufuli leo tarehe 02 Januari, 2019 amemjulia hali Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Salim Ahmed Salim ambaye anapatiwa matibabu Jijini Dar es Salaam baada ya kufanyiwa upasuaji.

Pamoja na kutoa pole kwa Dkt. Salim, Rais Magufuli akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli ameongoza sala ya kumuombea kwa Mwenyezi Mungu ili apone haraka.

Dkt. Salim alilazwa hospitalini jana na hali yake inaendelea vizuri.