Wakala wa maji vijijini kuanzishwa

0
970

Katibu Mkuu Wizara ya Maji Profesa Kitila Mkumbo amesema serikali imedhamiria kuanzisha wakala wa maji vijijini kwa lengo la kuharakisha utekelezwaji wa miradi ya maji vijijini.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dodoma Profesa Mkumbo amesema utaratibu wa kuanza kwa wakala huo umefikia hatua ya kupata maoni ambayo yatawezesha azma ya serikali kuanzisha wakala huo kutimia ili kukabiliana na changamoto ya maji vijijini.

Aidha Katibu Mkuu huyo wa wizara ya maji ametoa pongezi kwa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira kwa kuwa mamlaka bora ya utoaji huduma ya maji katika nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika.

Hata hivyo Prof. Mkumbo amesema Wizara ya Maji inaendelea kusimamia miradi ya nchi nzima ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji katika maeneo yao.